Kwa mujibu wa shirika la kushughulikia majanga – NDMA, jamii za wafugaji zinaendelea kubeba mzigo mkubwa wa athari za mabadiliko ya tabianchi baada ya mvua za vuli zilizotarajiwa kunyesha kati ya Oktoba hadi Desemba mwaka uliopita, kukosa kunyesha katika maeneo mengi ambayo hushuhudia ukame – ASAL.
Kama sehemu ya hatua za kuingilia kati, maafisa wa Shirika la Utafiti wa Kilimo na Mifugo Kenya (KALRO) wakiongozwa na Mkurugenzi Mkuu Dkt. Patrick Kiretien, wamehusishwa kusaidia juhudi za kusambaza chakula cha mifugo katika maeneo yaliyoathiriwa, hatua inayotarajiwa kupunguza hasara zaidi kwa wafugaji, serikali ikitakiwa kuanza kununua mifugo hao ili kuchinjwa kuepukea hasara.
Kadhalika, Shirika la Kitaifa la Msalaba Mwekundu, kwa ushirikiano na wadau wake, unaendelea kusambaza maji, chakula na msaada wa fedha taslimu kwa familia zilizo hatarini ili kuwasaidia kukabiliana na hali inayozidi kuwa mbaya.
Kwa kuwa utabiri wa hali ya hewa unaonyesha kuwa angalau miezi miwili ijayo itakuwa na mvua kidogo au kutokuwepo kabisa kwa mvua, mamlaka zinaonya kuwa hali ya ukame huenda ikaendelea kuwa mbaya zaidi endapo hatua za dharura hazitaimarishwa.
Wakati mjadala kuhusu siasa za eneo la Kaskazini Mashariki ukiendelea, waziri huyo aliongezea kuwa “kipaumbele cha serikali kwa sasa ni kuandaa na kutekeleza hatua za dharura ili kuhakikisha hakuna Mkenya, kutoka sehemu yoyote ya nchi, anayepoteza maisha kutokana na uhaba wa chakula.”
Katika ukanda wa Isiolo–Garissa–Meru, changamoto hizi zimechangia uhamaji wa wakazi na mifugo wao, na kudidimiza maendeleo.
Msafara huo unaoendeshwa chini ya kaulimbiu “Tudhibiti ukame, kwa amani na malisho endelevu,” ukiwa na lengo la kuhamasisha kuishi kwa amani na kuhakikisha mgawanyo wa haki wa rasilimali asilia, unatarajiwa kufanyika kuanzia Februari 2 – 5, 2026.